SIR ALEX FURGASON anfikilia nini na manchester united...!!!!
Ferguson anafikiria nini na united
yake?
NA BARAKA MBOLEMBOLE
Sir Alex Ferguson, mpende kocha huyu, lakini pia unaruhusiwa kutompenda. Kama usipoegemea upande wowote wa kishabiki huyu ni mtu
Mama yake mzazi atampenda na kumuona mtoto bora. Lakini hiyo inamtambulisha
kama mtu 'ngangari' kinoma katika mchezo wa soka kote England na
duniani. Rekodi zake zinazungumza zenyewe, na mara nyingi amekuwa akitwaa
mataji ya ligi kuu na Ulaya baada ya kuwa na uwezo wa kuibadili timu yake
kutoka 'goi goi' na kwenda nayo uwanjani uku akisoma nyakati na kutwaa makombe
kwa tamaduni za Ki-manchester United pekee. Mbinu zake ni za kipekee na vikosi
vyake ni kama uchawi, ukitazama namna United ilivyoitia presha Manchester City hadi dakika ya mwisho ya City
katika ligi kuu msimu uliopita bila shaka utaamini kuhusu haya nayosema. Baada
ya msimu wa bila taji na wengi wakidhani United ilikuwa na kikosi dhaifu,
Ferguson ameweka imani kubwa kwa wachezaji vijana katika kikosi chake cha
msimu, aliwakosa kwa sehemu kubwa ya msimu viungo Tom Cleverly na Anderson,
hawa ni viungo vijana ambao tayari wamepevuka kuwa wachezaji wa kikosi cha
lwanza, walifanya vyema wakati United iliposhinda mechi tatu ndani ya wiki tatu
dhidi ya timu kubwa za London msimu uliopita, United ilizifunga, Tottenham,
Arsenal na Chelsea ndani ya wiki tatu ikicheza ugenini. Kuumia kwa vijana hao
kulipeleke Michael Carrick na Ryan Giggs kurudishwa katika kikosi cha kwanza
kwa haraka, na hata aliporudi Darren Fletcher timu haikuwa bora na wakakumbana
na kipigo kitakatifu kutoka kwa City, United ikaanza kuporomoka na kutolewa
katika hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa. Lakini kimaajabu wakati ligi ikiwa
imepamba moto na United ikionekana kuongezeka ubora baada ya Paulo Scholes
kurejea uwanjani mara baada ya dirisha dogo la usajili, januari kufunguliwa,
Scholes akamfanya Carrick kurejesha kiwango kiasi fulani, uku Giggs akitumia
uzoefu wake kuzalisha mabao kvoka katikati ya uwanja au upande wa kusho,
Antonio Valencia alikuwa ni kama amefunguliwa 'kamba' katika winga ya kulia,
alikuwa mpiga pasi bora wa pili katika ligi kuu msimu uliopita japo alikuwa
majeruhi kwa nusu msimu. United ikawa juu ya City kwa tofauti ya pointi nane
mechi nne kabla ya ligi kumalizika, lakini tofauti ya mabao ikaamua bingwa
baada ya United kushindwa kuwa na 'ngome' imara. United ilikabiliwa na majeruhi
wengi sana
katika msimu ulipita, japo hiyo haiwezi kuwa sababu ya kukosa kwao kutwaa
ubingwa,lakini ilichangia. Wakati Rio Ferdinand alipokuwa anaangaika kuwa
'fiti' mlinzi mwenzake Nemanja Vidic alikuwa katika meza ya madaktari akitibiwa
matatizo yake ya goti. Bahati mbaya kwa Ferguson ni kwamba, japo, John Evans
amekuwa akicheza na wazoefu hao katika ngome kwa miaka sita bado
hajajitofautisha na wachezaji wa timu kama Stoke City, huyu ndiye alitakiwa kuziba
'viraka' katika ulinzi wa United msimu uliopita lakni alishindwa. CRISS
smalling ni mlinzi bora kwa walio chini ya miaka 24 katika ligi kuu (kwa
mtazamo wangu) lakini kinda huyu ana 'mwili wa plastic' ni mtu wa kuumia umia
mara kwa mara, lakini anapokuwa 'fiti' hucheza kama Garry Neville akicheza
namba mbili na hucheza kama Allesandro Nesta akicheza nafasi ya kati. Ferguson anaamini tayari
ana kikosi bora ambacho kinaweza kutwaa mataji makubwa. SHINJI KAGAWA Hidetoshi
Nakata alikuwa ni kipenzi sana cha Wajapan, nakumbuka nami niliwahi kununua
jezi timu ya taifa ya Japan kwa kiasi cha shillingi elfu sita na mia tano mwaka
2001 na ilikuwa na namba saba imeandikwa Nakata, Nakata alikuwa Mjapan wa
kwanza kucheza soka Ulaya na ndani ya mwaka mmoja akafanikiwa kusìnda
'scuddetto' akiwa na ASpOMA. Ferguson
alijaribu mara kadhaa kumtwaa Nakata lakini Roma hawakuwa tayari kumuuza. Soka
la Nakata likaanza kutawaliwa na majeraha na taratibu akapotea, lakini sasa
Wajan watakuwa na matumaini ya kumuona Kagawa akifikia mafanikio ya juu akiwa
na United. Tayari ametwaa mara mbili ubingwa wa Bundesliga akiwa na Borrussia Dortmund katika misimu
yake miwili barani Ulaya. Amepevuka na huyu ndiye anayatarajiwa kuwafanya Danny
Welbeck, Wayne Rooney na Javier Hernandez kufunga mabao, ametua United kwa kazi
ya kuchukua mipira kutoka kwa Carrick(ambaye amekabidhiwa timu) na kuipenyeza
kwenye 'mashimo'. Mechi ya ufunguzi dhidi ya Everton wikendi hii inaweza
ikamsumbua lakini, Kagawa amekuja United kugawa pasi na kufunga mabao.